Ninakusalimu katika Jina lipitalo majina yote, Jina la Yesu
Kristo, ninatumaini unaendelea vyema na ni mzima wa afya, ninamshukuru Mungu
kwa ajili yako na kwa ajili ya familia yako
Leo tena ni siku njema inayopendeza na Mungu ameiandaa ili
tuweze kuyasimulia matendo yake makuu na ya ajabu katika maisha yetu,
tunaendelea na somo letu la chunga sana ulimi wako kama ulisoma au haukusoma
somo la jana ⇒⇒⇒ bofya hapa kulisoma sababu limebadilika kuna mambo mapya
Tulipoishia….
Tunaendelea…
Ipo siri kubwa katika kutumia ulimi wako vizuri, pale
unapoaanza kuutumia vema mambo yanabadilika na kuwa mazuri, Mfalme Daudi
aliifahamu siri hii ndiyo maana
akamuomba Mungu aweke mlinzi kinywani mwake, ili asiongee mambo yasiyo na
msingi Zaburi 141:3 “Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojenzi mlangoni
pa midomo yangu
Mara nyingi sana watu wanaongea mambo ya kijinga kwa sababu
ya sehemu wanazokwenda na aina ya watu wanaoshirikiana nao, siku ukibadilisha
aina ya sehemu unazoenda na watu wasioelekea unapokwenda hata maneno yako
yatabadilika, kila sehemu zina maneno yake mfano bar kuna lugha yake, disko
kuna matendo yake Zaburi 39:1 “Nilisema, Nitazitunza njia zangu, Nisije
nikakosa njia zangu
Mfalme Daudi anasema mtu mbaya alipokuwa anakuja kwake
alikuwa hana muda wa kufungua kinywa chake, kwa maana nyingine ni kwamba alitia
gundi mdomo wake, hakuna kuongea na watu wajinga usije ukawa mjinga kama wao kwa
sababu mtu ni wastani wa tabia za marafiki zake sita anaokaa na kuongea nao
sana, anza kuangalia marafiki zako ondoa wale wasio na sababu Zaburi 39:1b
“Nilitia lijamu kinywani, Maadamu mtu mbaya awapo mbele yangu
Wakati ninamaliza kidato cha sita nilisema sitaki kwenda
kusoma elimu ya juu na watu niliosoma nao na nilimaanisha, nilisema maisha ni
safari ninataka kukutana na watu wengine sio kama hawa japokuwa tulisoma wote
shule moja ila hata sasa nina rafiki wawili tuu kati ya watu zaidi ya 60
tuliosoma pamoja
Nilifanya hivi kwa akili na nilijua ninaelekea sehemu fulani
sitaki mtu wa kunikatisha tamaa au kuniambia maneno nisiyoyahitaji, Mungu
anaanza kuongea na wewe pele unapojifunza maneno ya kuongea na kuwa na muda wa
kutosha kutafakari neno lake, namshukuru Mungu leo kwa sehemu aliyonifikisha na
vitu anavyovifanya kupitia mikono yangu na utumishi wangu
Kitu cha kwanza cha mtu anayejua kutumia ulimi wake ukikaa
naye hana muda wa kuongelea mambo ya watu, utamsikia akiongea juu ya maono
aliyokuwa nayo na jinsi anamwamini Mungu atamfikisha, kama unakaa na mtu dakika
thelathini kazi yake ni kuongea habari za wengine jua huyo hajui anakoelekea,
kifupi amepotea
Ulimi wetu ni kalamu japokuwa wengi hawafahamu unapoongea
unaandika katika ulimwengu wa roho tafadhali fahamu hili, tena ulimi unaandika
vizuri kuliko hata mikono yako, hakuna Mtumishi yeyote hata awe na nguvu kiasi
gani anaweza kutenda muujiza pasipo kuongea, ni mpaka unapotamka ndio mambo
yanatokea Zaburi 45:1 “Moyo wangu umeufinika kwa jambo jema, Mimi nasema
nilivyomfanyia Mfalme; Ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi stadi
Tambua ya kwamba watu wajanja ni wale wanaojua kutumia ndimi
zao vyema, sehemu sahihi na anasema neno sahihi, ushindi unaanzia kwenye
matamshi unayosema, Shetani hashindwi kwa mdomo uliofungwa bali kwa kumtamkia
neno la Mungu, yeyote anayekutakia mabaya mtamkie na wewe kabla hayajafanyika
kuwa kweli kwako
Zaburi 71:24 “Ulimi wangu nao utasimulia, Haki yako mchana
kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya
Nilishasema kwamba wokovu siyo ujinga, wokovu ni kujua haki
zako ukija kuleta ujinga kwangu ninakuwajibisha na mimi situmii mwili natumia
neno ndiyo maana ya kutofautishwa, ndiyo maana ukaitwa siyo mtu wa ulimwenguni
humu maana yake hata utendaji wako wa mambo ni tofauti kabisa na wa watu wa
ulimwengu huu
Ni jukumu letu kutumia ndimi zetu kunena sifa za Bwana kila
wakati, nilisema kwamba kama kila siku wewe ni mtu wa kuomba tuu maana kuna
watu hawaoni vitu walivyonavyo kila siku wanajiona wamepungukiwa kama upo hivi
jua una matatizo, kumpa Mungu sifa ni sehemu muhimu kuliko zote kwenye maisha
yako
Wewe ni mtu wa namna gani huoni zuri hata moja la kumsifu
Mungu? Vipi afya, vipi ulinzi, vipi familia yako yaani kweli huoni? Badili huo
ulimi sasa tumia muda mwingi kusifu kuliko kuomba, au umesahau ukisifu mambo
yanazidishwa? Kumsifu Mungu ni
kutambua uweza wake katika maisha yako Zaburi 35:28 “Na ulimi wangu utanena
haki yako, Na sifa zako mchana kutwa
Itoshe sasa anza kumuita Mungu kwa kinywa chako, muambie
unampenda na unalipenda neno lake, mwambie upo tayari kusikia kutoka kwake na
utaona mambo yakibadilika kuwa mazuri kwako, Zaburi 66:17 “Nilimwita kwa kinywa changu…..
Itaendelea tena.....
Baba/kaka / mama/ dada/ Yesu Kristo anakuita tena leo anakuambia njoo uisikie sauti yangu nami nitakuponya na kukuondolea maangamizo yote
Kama amenibadilisha mimi na wengine wengi nina uhakika hata wewe anaweza kukubadilisha, haijalishi unapitia magumu gani muda huu lakini wakati wa uliokubalika ni sasa na ni kwa ajili ya maisha yako mwenyewe, kama unakubaliana nami fuata sala hii fupi ya toba sema;
SALA YA TOBA
Bwana Yesu ninakuja mbele zako mimi....................(taja jina lako) ninakiri kwamba nimekutenda dhambi na ninastahili kuhukumiwa
Kama amenibadilisha mimi na wengine wengi nina uhakika hata wewe anaweza kukubadilisha, haijalishi unapitia magumu gani muda huu lakini wakati wa uliokubalika ni sasa na ni kwa ajili ya maisha yako mwenyewe, kama unakubaliana nami fuata sala hii fupi ya toba sema;
SALA YA TOBA
Bwana Yesu ninakuja mbele zako mimi....................(taja jina lako) ninakiri kwamba nimekutenda dhambi na ninastahili kuhukumiwa
Lakini kwa sababu wewe ni Mungu mwenye rehema na neema naomba unisamehe, unioshe na kunisafisha kwa damu yako ya thamani uliyoimwaga pale msalabani
Ninaomba ufute jina langu kwenye kitabu cha hukumu na uliandike kwenye kitabu cha uzima, karibu Yesu ndani yangu ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya. Ahsante Yesu kwa kuniokoa Amen.
Hongera, kwa kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, huu ni mwanzo mpya wa maisha yako ndani ya Kristo Yesu
Na kwa kuwa umetamka maneno hayo kwa imani wewe ni kiumbe kipya kumbuka unahitaji kujijenga kiroho zaidi tuna mafunzo maalumu kwa ajili yako wasiliana nasi kwa simu nambari/ Whatsup 0715113636 ili tuendelee kukuombea na kukushirikisha neno zaidi, Mungu akubariki sana
Kama unatamani kuwa mmoja wa wanachama wa Mwanamke Thamani (MT) na kujiunga nasi kuomba, kujifunza neno la Mungu kwa pamoja kama familia moja tunakukaribisha sana waweza kuwasiliana nasi kwa whatsup nambari 0715113636
Ninaomba ufute jina langu kwenye kitabu cha hukumu na uliandike kwenye kitabu cha uzima, karibu Yesu ndani yangu ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya. Ahsante Yesu kwa kuniokoa Amen.
Hongera, kwa kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, huu ni mwanzo mpya wa maisha yako ndani ya Kristo Yesu
Na kwa kuwa umetamka maneno hayo kwa imani wewe ni kiumbe kipya kumbuka unahitaji kujijenga kiroho zaidi tuna mafunzo maalumu kwa ajili yako wasiliana nasi kwa simu nambari/ Whatsup 0715113636 ili tuendelee kukuombea na kukushirikisha neno zaidi, Mungu akubariki sana
Kama unatamani kuwa mmoja wa wanachama wa Mwanamke Thamani (MT) na kujiunga nasi kuomba, kujifunza neno la Mungu kwa pamoja kama familia moja tunakukaribisha sana waweza kuwasiliana nasi kwa whatsup nambari 0715113636
No comments:
Post a Comment
Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana