Ukisoma habari za Adamu na Hawa baada
ya kumkosea Mungu utagundua kwamba swali la kwanza ambalo Mungu alimuuliza Adam
ni hili Adam upo wapi? Hii haimaanishi Mungu hakufahamu Adamu alipokuwepo
wakati ule ila alitaka akiri kwa kinywa chake sehemu ambayo aliyokuwepo.
Ukipigiwa simu na upo katikati ya mji
na ukaulizwa uko wapi kama sehemu hiyo haifahamiki lakini mbele yake kuna
sehemu maarufu utaitaja hiyo au jengo maarufu kisha utamwambia ulipo.
2Kor 9:10 “Na yeye ampaye
mbengu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na
kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu katika
kipindi hiki cha kupanda mbegu mtizamo unaoingia nao shambani una mchango
mkubwa sana katika mavuna utakayoyapata, kama unapanda tuu mbegu alimradi
umepanda na hauna matarajio ya ushindi mkubwa basi matokeo yako yatakuwa hafifu
Umeamua kuanzisha biashara amini
asilimia mia moja utafanikiwa katika biashara hiyo kuliko watu wengine wote,
umeajiriwa katika taasisi fulani amini utakuwa mfanyakazi bora na hakuna
atakayefanya vyema kama wewe
Baba yangu mzazi huwa ana Imani yake
kwamba kila akienda kupanda mbegu shambani ni lazima usiku wake au siku
inayofuata jioni mvua inyeshe, na amekuwa akiamini hivi kwa miaka mingi na
ndivyo inavyokuwa kwake, watu walikuwa wakimpigia simu na kumuuliza lini
anapanda mbegu ili nao wapande nae sababu ni kitu ambacho wamekuwa wakiona kinatokea
kwake miaka kadhaa Math 9:29 “Ndipo alipowagusa macho akisema, Kwa kadiri ya Imani yenu
mpate utapata kadiri ya Imani yako siyo kadiri ya machozi na masononeko
Kitu cha msingi hapa ni kwamba kama
hujui ulipo huwezi kufahamu unakoelekea, hivyo kwenye maisha utakutana na watu
wengi sana ambao wanavutiwa na sehemu uliyopo lakini swali kubwa na la msingi
la kujiuliza ni jee hiyo ndiyo sehemu Mungu anataka uwe?
Katika kipindi hiki cha kupanda mbegu
unapaswa kuwa mtu wa kuwekeza kila shilingi ambayo unaipata na pia ndio kipindi
cha kujitoa sana, ni lazima upande mbegu zako shambani kisha uhakikishe kwamba
zinapata mvua/maji, zinapaliliwa na kuondolewa magugu ndipo utakapoweza kuvuna
mazao mazuri
Hatuanzishi biashara tukaiacha kwa
wafanyakazi kabla haijashamiri na kuhakikisha ina usimamizi uliotukuka, wengi
hufikiri wanapaswa tuu kuanzisha biashara wanasahau biashara siyo kuanzisha,
biashara ni kuisimamia na kuiwekea misingi mpaka iweze kuleta faida maradufu
Kadhalika na kwenye Idea/wazo letu ni
lazima tuhakikishe tunalipangilia vizuri, tunashirikisha watu sahihi ambao
wataondoa magugu kisha tunazipanda kwa kuzitendea kazi, kuwa na mbegu ni kitu
kingine na kupanda mbegu mpaka imee na kuzaa ni kitu kingine kwa sababu kuna
michakato ambayo itapitia mpaka ifikie inapopaswa kufika.
Maisha ni magumu kama kila kitu
tutataka kufanya peke yetu bila kutafuta msaada wa kimaarifa, kutengeneza
mahusiano na watu fulani na kuwa tayari kujifunza yale ambayo tunaelekezwa na waliotutangulia
Kuna watu ambao wameshafika unakoelekea, ni hekima kuwasikiliza kuliko kuwadharau na kutaka kufanya njia kuwa refu, uzuri wa kujifunza kwa aliyekutangulia ni kwamba unaachana na changamoto alizopitia unachukua vitu alivyovifanya vikamfanikisha tuu
Ni muhimu tukatambua kwamba sisi
tulikuwa ni wazo la Mungu kisha tukaumbwa, lakini kwenye kuumbwa kwetu Mungu
aliweka viungo mbalimbali katika miili yetu na vinapofanya kazi kwa pamoja
ndipo tunapokuwa wazima.
Hitilafu ya kiungo kimoja mfano figo
inaonekana mpaka kwenye ini na mapafu hivyo kila kiungo kina umuhimu wake,
usikae ujidanganye na kujiambia kwamba unaweza kufanya kila kitu peke yako Mith
28:26 “Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga; Bali yeye aendaye kwa busara
ataokolewa kila wazo tulilonalo hatuwezi kulimaliza peke yetu kuna
ladha ya mtu fulani itahitajika kiutendaji, kuna ushauri utahitajika, kuna
fedha zitahitajika n.k
Itaendelea tena .....!
Ninaomba ufute jina langu kwenye kitabu cha hukumu na uliandike kwenye kitabu cha uzima, karibu Yesu ndani yangu ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya. Ahsante Yesu kwa kuniokoa Amen.
Hongera, kwa kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, huu ni mwanzo mpya wa maisha yako ndani ya Kristo Yesu
Na kwa kuwa umetamka maneno hayo kwa imani wewe ni kiumbe kipya kumbuka unahitaji kujijenga kiroho zaidi tuna mafunzo maalumu kwa ajili yako wasiliana nasi kwa simu nambari/ Whatsup 0715113636 ili tuendelee kukuombea na kukushirikisha neno zaidi, Mungu akubariki sana
Kama unatamani kuwa mmoja wa wanachama wa Mwanamke Thamani (MT) na kujiunga nasi kuomba, kujifunza neno la Mungu kwa pamoja kama familia moja tunakukaribisha sana waweza kuwasiliana nasi kwa whatsup nambari 0715113636
Baba/kaka / mama/ dada/ Yesu Kristo anakuita tena leo anakuambia njoo uisikie sauti yangu nami nitakuponya na kukuondolea maangamizo yote
Kama amenibadilisha mimi na wengine wengi nina uhakika hata wewe anaweza kukubadilisha, haijalishi unapitia magumu gani muda huu lakini wakati wa uliokubalika ni sasa na ni kwa ajili ya maisha yako mwenyewe, kama unakubaliana nami fuata sala hii fupi ya toba sema;
SALA YA TOBA
Bwana Yesu ninakuja mbele zako mimi....................(taja jina lako) ninakiri kwamba nimekutenda dhambi na ninastahili kuhukumiwa
Lakini kwa sababu wewe ni Mungu mwenye rehema na neema naomba unisamehe, unioshe na kunisafisha kwa damu yako ya thamani uliyoimwaga pale msalabani
SALA YA TOBA
Bwana Yesu ninakuja mbele zako mimi....................(taja jina lako) ninakiri kwamba nimekutenda dhambi na ninastahili kuhukumiwa
Lakini kwa sababu wewe ni Mungu mwenye rehema na neema naomba unisamehe, unioshe na kunisafisha kwa damu yako ya thamani uliyoimwaga pale msalabani
Ninaomba ufute jina langu kwenye kitabu cha hukumu na uliandike kwenye kitabu cha uzima, karibu Yesu ndani yangu ya kale yamepita na tazama yamekuwa mapya. Ahsante Yesu kwa kuniokoa Amen.
Hongera, kwa kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, huu ni mwanzo mpya wa maisha yako ndani ya Kristo Yesu
Na kwa kuwa umetamka maneno hayo kwa imani wewe ni kiumbe kipya kumbuka unahitaji kujijenga kiroho zaidi tuna mafunzo maalumu kwa ajili yako wasiliana nasi kwa simu nambari/ Whatsup 0715113636 ili tuendelee kukuombea na kukushirikisha neno zaidi, Mungu akubariki sana
Kama unatamani kuwa mmoja wa wanachama wa Mwanamke Thamani (MT) na kujiunga nasi kuomba, kujifunza neno la Mungu kwa pamoja kama familia moja tunakukaribisha sana waweza kuwasiliana nasi kwa whatsup nambari 0715113636
No comments:
Post a Comment
Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana