MRUHUSU MUNGU APIGANE VITA VYAKO - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Sunday, January 28, 2018

MRUHUSU MUNGU APIGANE VITA VYAKO

Zipo nyakati katika maisha unaweza kupitia mambo magumu, unaangalia nyuma unaona giza totoro unaangalia mbele unaona giza inakuwa kama huoni unakoelekea

Haupaswi kuogopa maana Biblia inasema Isaya 41:10 "Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu"

Kama hukusoma makala iliyopita ya Tujifunze kushukuru tafadhali Gusa hapa

Jambo jingine kubwa nililojifunza kipindi hiki ni kuhakikisha unaimarisha zaidi mahusiano yako na Mungu
Anasema katika 1Petro 5:6-7 "Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu

Haijalishi ni jambo gani unapitia wewe nyenyekea chini ya mkono wake sababu yeye ni hodari na yupo  kwa ajili yako

Wakati ambao hujui ni nini cha kufanya wewe msifu Mungu, haijalishi ni jambo gani gumu unapitia hakikisha unamsifu Mungu, unapata muda wa kutosha kusoma neno lake na kuomba

Mungu anasema katika 1Mambo ya walawi 16:25 " Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana; Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote."

Katikati ya giza tororo watu wote wamelala Daniel, Meshaki na Abelnego wanaanza kumsifu Mungu na hawakuuwawa asubuhi iliyofuata

Unapomsifu Mungu tegemea Mungu kupigana kwa ajili yako, ukitaka kumuona Mungu akiwa kazini msifu na kumwabudu kutokea moyoni

Mungu anapenda kusifiwa na kupewa namba moja katika kila kitu tunachokifanya sababu ametuumba ili tumuabudu,tulisifu na kulitukuza jina lake

Siyo kila vita unapaswa kupigana wewe, vingine siyo saizi yako hivyo utapigwa tuu, unapaswa kumsifu Mungu na kumuomba aingie katikati ya vita vyako

Ninaposema Mungu kupigana kwa ajili yako usifikiri atashuka na kuchukua upanga au bunduki la hasha! Mungu atainua watu ambao watakuwa upande wako, Mungu atakupa Idea mpya za kutatua changamoto unazozipitia, Mungu atakuheshimisha mbele za watu

Unamkumbuka Mfalme Jehoshafati 2Mambo ya Walawi 20:19-- alishinda vita pasipo hata kupigana waaza kusoma habari yake zaidi ukiwa faragha na neno la Mungu

Sababu kubwa ya Mungu kupigana kwa ajili yetu ni kwamba maadui wetu ni wengi sana, vita havijaisha mpaka Mungu aingie katikati ya vita kwa ajili yako

Unapomruhusu Mungu kuingilia vita vyako anakuwa adui wa adui zako Kutoka 23:22 " Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao"

Pindi Mungu anavyopigana kwa ajili yako vita huisha anasema Kumb la Torati 20:4 "Kwa maana BWANA, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi
"
Mungu anapoingilia vita vyako wewe unakuwa mtazamaji na siyo mpiganaji 

Anakuinua kutoka utukufu mpaka utukufu na analifanya suala lako kuwa la tofauti

Siyo lazima upigane ndio ushinde, acha Mungu apigane kwa ajili yako jua kwamba siyo wapiganaji wote hupigana, wenye hekima pindi vita vinavyokuwa vigumu sana kwao humuacha Mungu kupigana kwa ajili yao

Kuna watu wanayaangalia matatizo wanayavaa mpaka wao wenyewe wanakuwa matatizo

Kumsifu na kumtukuza Mungu kunaondoa vizuizi vyote vya sisi kufikia mafanikio yetu

Jikabidhi kwa Mungu mwache aingilie kati vita vyako nawe utakuwa umevipiga vita vizuri na kuumaliza mwendo salama

NB: Maneno Vita / adui kama yalivyotumika yaweza kuwa ni matatizo, ugumu, changamoto ambazo tunazipitia katika maisha yetu

Kama bado hujasubscribe you tube chanel ya MWANAMKE THAMANI  Gusa hapa Tafadhali   kumbuka leo saa kumi na moja kamili jioni ndio tunaweka kipindi cha kwanza hivyo ili usipitwe hakikisha unasubscribe mapema

Mwanamke Thamani! "Wewe umewazidi wote"

No comments:

Post a Comment

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana