Ulimi ni kiungo kidogo sana lakini kinaweza kukuletea faida au madhara
kulingana na namna ambayo utakuwa unakitumia, wengine wamekuwa wanatumia ndimi zao kulaani wengine na kujitamkia laana na maneno ya kukatisha tamaa, lakini wapo ambao wanatambua matumizi ya ndimi zao wanazitumia kubariki na kujitamkia maneno ya baraka
Kuangalia video ya kipindi cha pili cha Mwanamke Thamani cha Nguvu ya Ulimi angalia video iliyopo juu kabisa au GUSA HAPA
1Petro 3:10 "Kwa maana, atakaye kupenda maisha, na kuona siku njema, auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila"
Kiuhalisia siyo matukio au hali ya hewa ndiyo inayoharibu siku bali ni namna ambavyo tunatumia ndimi zetu na midomo yetu kuongelea kilichotokea au kitakachotokea katika siku husika
Kila kitu kina uzuri wake lakini ukikaa kutafuta ubaya badala ya wema na kutumia ulimi na mdomo wako kuongelea hayo basi hata siku yako itakuwa mbaya na iliyokosa baraka
Biashara, kazi, mahusiano, udugu hujengwa kwa ulimi, namna ambayo unaongea na wateja wako, unavyoongea na familia yako, mkuu wako wa kazi na watendakazi wenzio ndio itaamua ufanikiwe au ubomoe unachokifanya
Binadamu tumekuwa tunaongea maneno mabaya, maovu ya kukatishana tamaa na kujiambia kwamba hatuwezi kufika sehemu fulani au hatuwezi kufanikisha suala fulani lakini tunasahau kwamba kile ambacho tunakikiri kwa ulimi na midomo yetu ndicho ambacho hutokea
Kama haukusoma makala iliyopita ya ULE MSHAWASHA UTAKAOTOKEA GUSA HAPA
Neno ni sawa na kiapo, ndiyo maana viongozi huapizwa kwa maneno na kwa mujibu wa dini zao, Amini Amini nakuambia hakuna sababu yeyote ya kusema jambo ambalo haulitaki maishani mwako
Kama unataka utajiri usikae ukae chini na kukiri wewe ni masikini na huwezi kufanikiwa, kama unataka kuwa na mahusiano mazuri na watu usikae useme fulani anaringa na hataki kushirikiana na watu, kama unataka mafanikio kielimu usikae useme nitafeli somo fulani au mimi ni dhaifu sehemu fulani, kiri na tamka tena kwa ujasiri kitu ambacho unakihitaji pekee
Hii ndiyo maana Biblia ikasema katika Waefeso 4:29 "Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia"
Una kila sababu ya kutamkia watu habari njema na za kufurahisha, una kila sababu za kuwabariki watu kwa kile ambacho Mungu amekupa, kiuhalisia hakuna mtu mbaya hata mmoja duniani kila mtu ana uzuri wake kabla ya kuangalia ubaya tafuta uzuri na utamke
Kumbuka kabla ya ombi lolote huanza shukurani na pongezi haijalishi hali ilikuwaje ndipo mengine hufuata baada ya kushukuru na kukipongeza kile kilichopo
Mwanamke Thamani "Wewe umewazidi wote"
TV Online Channel
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment
Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana