UPONYAJI WA FAMILIA - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Wednesday, July 18, 2018

UPONYAJI WA FAMILIA


Jana tuliangalia umuhimu wa kuwa na umoja katika familia, leo tunaenda kuangalia uponyaji katika familia 

Kama hukusoma sehemu ya nne ya mfululizo wa makala hii ya familia juu ya umuhimu wa umoja ⇉⇉⇉⇉ GUSA HAPA KUISOMA

Ninaposema uponyaji usiyeyushe au kufupisha maana uponyaji ni neno pana siyo lazima iwe ni ugonjwa katika mwili inaweza kuwa ni uchumi, ndoa, vifungo, ugonjwa n.k lakini kwa mada hii niongelee uponyaji kwenye magonjwa

Katika kanisa leo hii kuna wagonjwa na watu waliofungwa katika vifungo mbalimbali, hatuwezi kulilaumu kanisa au uongozi ndio maana karama zikawepo mbalimbali zinazosaidia kanisa katika kutimiza kusudi la Mungu

Upungufu wa watumishi na wingi wa vifungo na hila za Shetani ni moja kati ya sababu inayopelekea kuongezeka kwa watu wengi waliofungwa na wanaokwenda huku na kule kutafuta uponyaji

Lakini pia kutokuelewa mpango wa Mungu na asili ya Mungu imekuwa ni moja ya sababu kubwa ya magonjwa na vifungo kwa Wakristo wengi

Uponyaji ni fungu letu na ndio kusudi la Yesu Kristo kufa lakini Shetani amebadilisha maana na kuwaaminisha watu kuumwa au kufungwa katika sehemu fulani ni sehemu ya maisha

Kuwa na afya ni bora kuliko kuponywa ukumbuke sisi ni mfano wa Mungu na kama ni hivyo na unaamini basi unao uwezo wa kuidai afya yako ya kiungu

Mungu anataka kila mtu awe na afya yake kuliko kuponywa ndio maana akasema 
3Yohana1:2 "Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.

Shetani baba wa hila hajawahi kuumba kitu uzima na afya viliumbwa na Mungu yeye akapindisha kwa sababu ya hila akaleta magonjwa na vifungo

Ugonjwa au vifungo siyo fungu letu kwa sababu yupo Simba wa Yuda ambaye alishalipia gharama ya mateso yote ambayo yanamuandama binadamu ndio maana neno la Mungu linasema katika Isaya 53:5 "Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona

Wakati fulani mtumishi mmoja alikuwa akihubiri na akasema watu wote ambao ni wagonjwa ni wezi, hii sentensi ilinishangaza lakini aliendelea kuelezea hoja yake na kuonesha kusudi la Yesu kuja akasema kama Yesu aliyachukua maovu yetu na tabu zetu na kwa kupigwa kwake sisi tumepona sasa magonjwa watu wanayapatia wapi kama siyo wezi?

Mungu anasema kwamba tukimtumikia Kutoka 23:25 "Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.

Je magonjwa yanatoka wapi?

Tumeona Shetani hajawahi kuumba kitu chochote Mungu aliumba afya na uzima Shetani akapindisha akaleta magonjwa na kifo

Magonjwa kifupi yanatokana na mambo makuu matatu

Jambo la kwanza ni Uovu, uovu ni dhambi ambayo imekomaa hata ikapita kutoka kizazi kimoja hata kingine dhambi hii hufungua milango ya magonjwa na mahangaiko mf babu zako wanaweza kuwa sababu ya magonjwa ulionayo

Uovu unaweza kusafiri kupitia cheneli zifuatazo inawezekana kwenye dhambi inayojulikana au isiyojulikana, nadhiri, viapo vinavyohusisha damu, nchi kwa watu wake kwa mfano Jer 3:6-10, kuasi, kurithi kwa wazazi mwanz 16:1 pia inawezekana kupitia majina 1Nyak 4:9-10

Jambo la pili ni Laana, laana ni tamko hasi ambal husemwa kwenye maisha ya mtu, familia, kundi la watu au nchi ukisoma Biblia kuna mtu alikuwa anaitwa Baalam huyu alikuwa kazi yake ni kutamka laana kwa Watumishi wa Mungu

Jambo la tatu ni dhambi, hii ni kwenda kinyume na neno la Mungu siri ni hii laana na uovu unaendelea kuwepo kwenye maisha ya mtu au familia fulani alimradi tuu wanafanya dhambi

Unapotubu na kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako unajiweka katika nafasi nzuri ya kuiondoa laana na uovu na ndio maana wokovu ni jambo la kwanza kabisa kwa binadamu

Tufanyeje sasa kama tunaumwa?

Tunapaswa kuidai afya yetu kwa nguvu suala la kudai haki na stahiki zako siyo lelemama ni mapambano ndio maana Mathayo11:12 inasema "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

Haukai kuongea maneno na kutangaza kwamba naumwa naumwa kwa kila mtu bali unazivaa silaha unaingia kwenye ulimwengu wa Roho unapigana kuidai afya yako ya kiungu

1Kor 4:20 "Maana ufalme wa Mungu hauwi katika neno, bali katika nguvu, hizi nguvu siyo za mwili ni za Kiroho hivyo ni lazima kujijenga katika eneo la Kiroho hata Kiuchumi

Instagram @Mwanamkethamani

Kama una shauku na hamu ya kujifunza neno la Mungu pamoja na kujiunga na network ya wanawake ambao kwa pamoja tunamtumikia Mungu na kujifunza juu ya kusudi ambalo Mungu ameweka maishani mwetu unaweza kuwasiliana nasi kwa simu nambari 0715113636

Mwanamke Thamani "Wewe umewazidi wote"

©mwanamkethamani articles gallery use under permission only

No comments:

Post a Comment

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana