HIKI NI KIPINDI CHA KWARESMA - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Tuesday, February 20, 2018

HIKI NI KIPINDI CHA KWARESMA



Tupo kwenye majira ya kwa resma ambayo Wakristo hufunga na kuomba kwa sababu tunakumbuka kipindi ambacho Yesu mwana wa Mungu aliteswa na kusulubishwa kwa ajili ya dhambi zetu

Kipindi hiki kinatukumbusha majira ya mwisho wa safari ya Bwana wetu Yesu Kristo katika kuhubiri habari njema ya wokovu na kukombolewa kwa watu wenye dhambi  kutoka kwenye maovu yao, katika kipindi hiki tunajutia dhambi zetu, tunaungama na tunajitakasa

Kama haukusoma makala ya Upepo hauamui uelekeo wa meli unaweza Kugusa Hapa ukaisoma yote 

Tunakumbuka kwamba Wanawake ndio walikuwa mstari wa mbele kwenye safari hii ya mateso ambayo Yesu aliiendea kipindi kile na hata wakati anateswa na kusulubishwa bado walikuwepo hata alipokufa na kufufuka walikuwa wa kwanza kuona kwamba jiwe lililokuwepo kaburini mwa Yesu halipo tena

Team ya Mwanamke Thamani nasi  tumeamua kutumia kipindi hiki vyema kwa kufunga, kuomba  na kujitakasa tukiungana na  Wakristo wengine ulimwenguni kote ambao nao wanafanya vivi hivi, hii ni moja ya sababu ya kwa nini tumekuwa kimya mwezi huu

Pia tunajiandaa kwa ajili ya tamasha la  BINTI JITAMBUE linalofanyika Mwanza kuazia tarehe 8-10 mwezi wa tatu, Mwanamke Thamani ikishirikiana na Ev.Tedy Stephen tunaandaa Kongamano la maombi na maombezi ambalo litafanyika tarehe 30 na 31 mwezi wa tatu jijini Dar

Wengi watafunguliwa na kupona, watauona ukuu na uweza wa Mungu katika maisha yao, tunakukaribisha katika Kongamano hili la kipekee na litakalokuwa na mguso wa aina yake, njoo na wewe na familia yako, ndugu, jamaa, rafiki taarifa juu ya eneo tutasema hapo baadae ili kwa muda huu unaweza kuwasiliana na timu nzima ya maandalizi kwa ..

Ev.Tedy Stephen               0754-563-253 ⇣⇣⇣⇣⇣⇣⇣

Mwl. Sialove Lukumay      0715-113-636 ⇣⇣⇣⇣⇣⇣

Mwl .Pendo  Emmanuel    0755- 715-715 ⇣⇣⇣⇣⇣⇣

Mwanamke Thamani "Wewe umewazidi wote"

No comments:

Post a Comment

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana