Tumeshajifunza kwamba ni vigumu sana watu ambao mmelelewa mazingira tofauti kukaa pamoja bila kukoseana, ni lazima mtakoseana kwa sababu ya utofauti wenu
Lakini tofauti baina yetu zipo kwa ajili ya kutujenga na kutuimarisha na siyo kutubomoa au kutuharibu ndiyo maana tunapaswa kufurahia utafauti wetu, kama jana haukusoma sehemu ya pili ya Nguvu ya msamaha Gusa hapa kuisoma
Kila mmoja ni imara sana katika eneo fulani na dhaifu katika eneo jingine, hali hii inaleta uhitaji wa mtu mwingine katika eneo lenye udhaifu
Ukiangalia kwa takwimu ugomvi na mfarakano kwenye ndoa kichocheo cha kwanza ni fedha na cha pili ni kukosekana kwa moyo wa msamaha kati ya wanandoa
Mara nyingi watu wamekuwa wanaingia katika mtego wa Shetani wa kumtamkia tuu mtu mdomoni nimekusamehe lakini ndani ya mioyo yao wana vidonda na wanabubujika machozi
Hivyo utakuta mtu akimkosea mwenzake anamuhesabia makosa anapokuja kumkosea tena anamwambia unakumbuka siku fulani ulinifanyia abcd.....
Tayari kwa kufanya hivyo moyo wake unajawa na hasira, chuki na huzuni kwa sababu hata mara ya kwanza hakuwa amesamehe kama alivyosema
Kusamehe haimaanishi kwamba unaigiza kama vile hukuwahi kukosewa bali ni unaachilia kile ulichokosewa kutokea ndani ya moyo wako
Kusamehe siyo jambo la akili bali ni suala la moyo na hii ndiyo maana inakuwa ni suala gumu na lenye kuhitaji upendo wa kimungu ambao upo mioyoni mwetu
Tunawezaje kusamehe?
Unapaswa kukumbuka kwamba wale ambao wamekukosea ni binadamu kama wewe na hakuna aliyemkamilifu, pengine hawakupenda kukukosea na pia hawajakamilika kuna siku na wewe utakosea na utahitaji msamaha kama wao
Yakobo 1:2 "Maana twajikwaa sisi sote katika mambo mengi, mtu asiyejikwaa katika kunena huyo ni mkamilifu....."
Unapaswa pia kufahamu kipindi unasamehe mtu aliyekukosea haufanyi dhambi bali unatimiza neno la Mungu, Mathayo 6:14-15 "Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi, bali msipowasamehe nanyi hamtosamehewa"
Tambua baraka ambazo utazipata kwa kusamehe, unapokuwa na kinyongo inakuwa ni vigumu kukuwa kiimani (spiritual growth) lakini unapoondoa kinyongo kunakufanya kutulia, utaimarika afya yako na utapata furaha pia
Mithali 14:30 "Moyo uliyo mzima ni uhai wa mwili bali husuda ni ubovu wa mifupa" wapo watu wamedhoofika afya na kuzeeka kabla ya muda wao sababu ya kushindwa tuu kusamehe
Mathayo 5:9 "Heri wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu" unaposamehe unajipatanisha na aliyekukosea na pia unajipatanisha na Mungu na kwa kufanya hivyo unapata sifa ya kuwa mwana wa Mungu
Kumbuka unakuwa unalipa jema kwa baya na hii ni baraka Luka 6:27 "Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, wapendeni adui zenu, na watendeeni mema wale wanaowachukia ninyi"
Mwanamke Thamani!
This series of Msamaha is amaizing thank you so much!
ReplyDelete