MTAZAMO CHANYA NI USHINDI-II - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Thursday, January 4, 2018

MTAZAMO CHANYA NI USHINDI-II



Ilipoishia jana....

Simoni na nduguze walichagua kutokufanikiwa kupata samaki baada ya kutupa wavu baaharini mara kadhaa na kushindwa kupata samaki

Kama hukusoma makala hii sehemu ya kwanza Gusa hapa


Twende sasa!

Katika maisha ya Ukristo unapoamua kufanya kitu na ukaona hakijaenda sawa kama ulivyotarajia haupaswi kabisa kukata tamaa wala kukuri kwamba umeshindwa

Wazo ni nguvu ambayo inasafiri na kupenyeza sehemu yeyote na muda wowote na wazo ndio linalopelekea kutokea kwa kitu chochote

Nyumba, magari, biashara, majengo makubwa na vyote tunavyoviona vimetokana na wazo fulani ambalo mtu alikuwa nalo kisha akalipangilia vizuri na kuanza kulifanyia kazi

Katika dunia hii hakuna kitu kinachotokea chenyewe, hata binadamu alikuwa ni wazo la Mungu, vitu husababishwa kutokea
Wazo unapoliwekea hisia unalipelekea katika hatua ya pili ya mtazamo na unapofanya hivi unasababisha akili yako kwenda kwenye mtikisiko mwingine katika akili ambayo haijalala huitwa hisia

Simoni na nduguze baada ya kujaribu kuvua samaki usiku kucha na kushindwa waliamua kuchagua kushindwa, kumbuka wazo ni hatua ya kwanza katika kutengeneza mtazamo

Baada ya hapo weliwekea wazo la kushindwa hisia za kutokupata samaki siku ile

Hisia zinapoanza kuwekwa kwenye vitendo au mazoea zinapelekea hatua ya tatu ya mtazamo 

Hapa tunajifunza kwamba hata utendaji kazi wa Simoni na nduguze ulibadilika na hali hiyo ndio iliyosababisha wasipate samaki siku ile

Hivyo basi mtazamo alionao mtu na matokeo havitengani, vinafuatana utafanya kama vile mtazamo wako utakavyokuwa

Ngoja niende mbali zaidi Yesu wakati anakuja katika vyombo vya kuvulia samaki vya kina Simoni na nduguze Biblia haisemi kwamba aliamuru samaki washuke kutoka mbinguni waingie kwenye nyavu zao

Wala hakuamuru samaki wa baharini waingie kwenye nyavu zao bali alisema tweka mpaka kilindini

Hivyo ni sawa nikisema tatizo la kukosa samaki lilisababishwa na mtazamo, Simoni na nduguze mtizamo wao uligeuka na kuamini wasingeliweza kupata samaki na ikawa hivyo 

Itaendelea........

No comments:

Post a Comment

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana