MLANGO - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Sunday, January 7, 2018

MLANGO



Ili uweze kuingia sehemu yeyote unahitaji kutafuta mlango wa kuingilia ulipo

Binadamu naye ana milango ambayo vitu hupita kupitia hiyo, milango mikuu ni miwili ambayo ni macho na masikio

Kitu chochote huingia akilini kupitia macho (kuona au kusikia), kadhalika kitu huingia mwilini kupitia mdomo

Hivyo tuna milango mbalimbali ulimwenguni ambayo ni;
a) Milango ya kiroho
b) Milango ya kidunia
c) Milango ya kimwili

Biblia inaposema mlango mwembamba ina maana mtu asiyekuwa na mambo mengi, mpana mtu mwenye mambo mengo 1petro 3:6
Yesu Kristo ndiye njia ya kweli na uzima (ndiye njia nyembamba itupelekayo uzimani) 

Unapokuwa kwenye mlango mpana unakosa hekima na maarifa sababu ni mlango unaoruhusu kila kitu hauchagui kila linalokuja unapokea

Tunapaswa kuishi kwenye mlango mwembamba tukimuogopa Mungu maana yeye ana majibu ya mambo yote

Mtu anayefanya maombi siyo wa kucheza naye kwa sababu anafanya mawasiliano na Mungu moja kwa moja

Mungu huangalia ni mlango gani umejifunga na kusababisha maisha yako kuharibika naye huufungua tena na kuachilia baraka zake

Huwa kuna chati za maombi kadiri unavyoomba chati yako hupaa hivyo tunapaswa kuomba zaidi kila iwapo leo

Maombi ni mtaji, biashara pamoja na kazi huaribika na huweza kufa pasipo maombi 

Hatuwezi kuuteka ulimwengu wa kiroho pasipo maombi, watu wengi hupenda kuombewa badala ya kujiombea wenyewe

Tunapaswa kuhama kutoka kiwango cha kupenda kuombewa na kujiombea wenyewe hapa ndipo tunapokuwa wana wa Mungu na siyo watoto wa Mungu

Watoto wanapofanya vibaya shuleni, usiwapige wala kuwalaumu jiulize mara ngapi umewaombe wao na rafiki zao

Wakati mwingine maombi yetu huzuiwa angani, unakumbuka wakati Daniel anasali Mungu alimwambia maombi yako Shetani aliyezuia yasinifikie?

Hivyo tunapaswa kupanda viwango vya kuomba ili tumshinde yule mwovu na hila zake

Kuna vijana watatu huwa napenda sana habari zao Shedraki, Meshaki na Abelnego, hawa watu walibadilisha nchi

Unajua haijalishi una elimu gani, urefu au ufupi gani, mnene au mwembamba lakini ukimtumikia Mungu anakuwezesha kufanya mambo makubwa na ya ajabu

Tunataka kuona nchi yetu inabadilika na milango mingine ya mafanikio ikitokea wa kuibadilisha na mimi na wewe

Usikae ujidharau wala ujione si chochote wewe ni mtu mkubwa na mwenye uwezo na maajabu


Mwanamke Thamani

1 comment:

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana