SIFA KWA BINADAMU NI KILEVI - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Thursday, January 4, 2018

SIFA KWA BINADAMU NI KILEVI



Wahenga wakasema "Sifa zinauwa" neno kuuwa siyo lazima roho ya mtu itoke inaweza kuwa ni vitu kuanza kwenda vibaya kama huduma kuharibika, biashara kufa, magonjwa kukuandama n.k

Kila binadamu anapenda kutambulika na kuthaminika kwa kile anachokifanya, lakini kutambulika hakupaswi kuwa kinyume na mpango na neno la Mungu

Binadamu akianza kujisifia/ kusifiwa na akalewa sifa na kumsahau Mungu sifa hizo humuuwa

Daudi rafiki wa Mungu angelikuwa anapenda sifa na kumsahau Mungu ndiye aliyemuwezesha yote haswa alipomuuwa Goliathi angalikufa mapema

Sifa anastahili kupewa nani?

Zaburi 145:3 Bwana ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana na wala ukuu wake hautambulikani, unachojisifia siyo chako ni Mungu kakupa mrudishie sifa

Ukijisifia sana mbele za watu na kuona umefanikisha huduma, biashara, mafanikio peke yako huna muda mrefu katika hilo unalojisifia litakufa

Wakati fulani niliandika Mungu hashei utukufu, kuna watu wanaowauwa watu kwa sababu wanawageuza watu hao kuwa mungu wao

Mungu hapendi wala hataki kusikia kitu chochote kinachukua nafasi yake katika maisha yetu, anapenda tumuweke namba moja katika kila kitu

2Samweli 22:4 Nilimuita Bwana astahiliye kusifiwa, hivyo nitaokoka na adui jibu linaonekana hapa anayestahili kusifiwa ni Mungu

Wapo watu wanaanzisha huduma zinafika mbali lakini wanafika sehemu wanajisahau, wanaona mafanikio yale ni juhudi zao na wanaanza kulewa sifa, jambo hili halimpendezi Mungu

Anguko la kitu chochote kile iwe ni biashara, huduma husababishwa na sifa, kukosekana kwa uongozi thabiti, kukosekana kwa hofu ya Mungu na kutojifunza mambo mapya

Binadamu anapewa pongezi, sifa anapewa Mungu Isaya 43:21 inasema watu wote niliowaumbia nafsi yangu wazitangaze sifa zangu

Habari ya tajiri mpumbavu aliyevuna mazao na akaweka ghalani, akasahau Mungu ndiye aliyemwezesha aliishia kufa usiku, kilochofanya afe ni kujisifu na kukosa shukrani kwa Mungu

Tukipenda tuishi vyema hatuna budi kufahamu mambo yanayomstahili mwanadamu na ya Mungu

Mwalimu, muimbaji, huduma, mwanamichezo ambaye anapenda sifa anguko lake hutokea mapema sana kabla ya wakati wake, ukiona mtu anafanikisha suala fulani kisha akaanza kujisifu anguko lake haliko mbali

Sifa ni kwa Bwana Yesu tuu!

No comments:

Post a Comment

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana