Tizama video hii
Kina mama wengi hubweteka baada ya kuolewa, wanasahau kabisa kwamba kusudi la kuolewa ni kuwasaidia waume zao
Sababu ya Mungu kumleta Hawa kwa Adamu ilikuwa ni kumfanya awe msaidizi wake
Kumsaidia mmeo siyo kwenye kupika, kufua, kusafisha nyumba tuu bali ni zaidi ya hapo ni mpaka kwenye maono yake
Mwanamke ameumbwa tofauti sana na mwanaume na anaweza kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja mwanaume hawezi
Hivyo mwanamke anapoambiwa na mmewe juu ya maono yake anayeyapanua ni mwanamke kwa kumuonesha njia nyingi zaidi za kuyakuza
Chunguza mwanamke utagundua kwamba kazi yake ni kukuza vitu ukimpa neno anakupa sentensi, ukimpa sentensi anakupa aya, ukimpa aya anakupatia kitabu kizima
Mwanamke alivyo wa ajabu ukimpatia mbegu tuu anaikuza tumboni anakupatia mtoto baada ya miezi tisa, hakuna kitu kinaenda kwa mwanamke kikarudi kama kilivyokuwa mwanzoni
Lakini dunia ya sasa wake wanabweteka na kuona kwamba wao wakishaolewa hawapaswi kufanya jambo jingine hivyo wanageuka mama wa nyumbani
Kazi yao ni kula, kujinyoosha, kuangalia tv, kufuga kucha, kusuka nywele, kupiga umbea na kulala
Unakuta mwanamke hajishughulishi hafanyi jambo lolote lile na imekuwa ni kawaida kwao anamuomba mmewe kila kitu hii siyo sahihi
Mwanamke anayefuga kuku ni mjasiriamali, anaekaanga maandazi na vitumbua ni mfanya biashara ndogo ndogo
Kataa kuwa mama wa nyumbani mwanamke unao uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo ya ajabu
Mwanamke Thamani
Baadhi ya wanaume ndio chanzo cha kuwafanya wake zao kuwa tengemezi au kubweteka.hawataki kabisa wake zao watimize ndoto zao/maono yao
ReplyDelete