MAMA WA NYUMBANI! - MWANAMKE THAMANI

TV Online Channel

Thursday, January 4, 2018

MAMA WA NYUMBANI!


Tizama video hii



Kina mama wengi hubweteka baada ya kuolewa, wanasahau kabisa kwamba kusudi la kuolewa ni kuwasaidia waume zao

Sababu ya Mungu kumleta Hawa kwa Adamu ilikuwa ni kumfanya awe msaidizi wake 


Kumsaidia mmeo siyo kwenye kupika, kufua, kusafisha nyumba tuu bali ni zaidi ya hapo ni mpaka kwenye maono yake

Mwanamke ameumbwa tofauti sana na mwanaume na anaweza kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja mwanaume hawezi

Hivyo mwanamke anapoambiwa na mmewe juu ya maono yake anayeyapanua ni mwanamke kwa kumuonesha njia nyingi zaidi za kuyakuza

Chunguza mwanamke utagundua kwamba kazi yake ni kukuza vitu ukimpa neno anakupa sentensi, ukimpa sentensi anakupa aya, ukimpa aya anakupatia kitabu kizima

Mwanamke alivyo wa ajabu ukimpatia mbegu tuu anaikuza tumboni anakupatia mtoto baada ya miezi tisa, hakuna kitu kinaenda kwa mwanamke kikarudi kama kilivyokuwa mwanzoni

Lakini dunia ya sasa wake wanabweteka na kuona kwamba wao wakishaolewa hawapaswi kufanya jambo jingine hivyo wanageuka mama wa nyumbani

Kazi yao ni kula, kujinyoosha, kuangalia tv, kufuga kucha, kusuka nywele, kupiga umbea na kulala

Unakuta mwanamke hajishughulishi hafanyi jambo lolote lile na imekuwa ni kawaida kwao anamuomba mmewe kila kitu hii siyo sahihi

Mwanamke anayefuga kuku ni mjasiriamali, anaekaanga maandazi na vitumbua ni mfanya biashara ndogo ndogo

Kataa kuwa mama wa nyumbani mwanamke unao uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo ya ajabu

Mwanamke Thamani

1 comment:

  1. Baadhi ya wanaume ndio chanzo cha kuwafanya wake zao kuwa tengemezi au kubweteka.hawataki kabisa wake zao watimize ndoto zao/maono yao

    ReplyDelete

Unaweza kutoa ushauri au kuwasiliana nasi kwa mafunzo zaidi, karibu sana